TAMWA: WAANDISHI TUMIENI KALAMU ZENU KUSAIDIA KUINUA  VIPAJI VYA MICHEZO VYA WANAWAKE.   




     
WAANDISHI wa habari za michezo kisiwani pemba wametakiwa kuongeza juhudi katika kuandika habari hizo kwa wanawake ili kuwezesha ushiriki sawa wa jinsi zote  kuzifikia fursa .

Ameyasema hayo Afisa tathmini na ufuatiliaji kutoka TAMWAZanzibar Mohammed khatib wakati wa kikao cha ufuatiliaji wa utendaji kazi kwa waandishi hao.

 “TAMWA inaamini waandishi wa habari wana uwezo mkubwa wakuhamasisha jamii katika harakati tofauti ikiwemo wanawake kwenye kushiriki michezo.”

“Mbali ya changamoto zinazowakabili wanawake katika kushiriki michezo ni vyema kwenu waandishi kuchukua changamoto mulizoziona kwenye jamii na kuzipeleka sehemu husika ili kushirikiana kuwasaidia  wanawake kushiriki michezo”aliongeza.

Akitaja lengo la tathmini hiyo afisa programu kutoka TAMWAZanzibar Khairat haji ali amesema ni kuangalia maendeleo ya mradi na kuweka taarifa za  matokeo ya mradi huo.

“Awamu iliyopita hali haikua nzuri ila kwa sasa inaridhisha, hivyo ni muhimu kuendelea ili kuhakikisha ushiriki wa wanawake kwenye michezo unaongezeka.”

Kwa upande Waandishi wa habari waliopo kwenye mradi huo wamesema bado changamoto za uhaba wa viwanja na mtazamo hasi kwa baadhi ya jamii pamoja na ushirikishwaji bado ni vizingiti kwa watoto wa kike kushiriki michezo.

“Baadhi ya wazazi wanatamani watoto wao washiriki michezo ila mazingira ya viwanja sio rafiki ya wao kushiriki michezo.” Alisema habiba zarali.

“Mavazi pia ni kikwazo kwa wazazi kuwaruhusu watoto wa kike kushiriki michezo.” Alisema fatma hamad.

Michezo kwa maendeleo ni mradi unaofadhiliwa na shirika la maendeleo ya kimataifa la Ujerumani( GIZ) na kutekelezwa na taasisi tatu @TAMWA_Zanzibar , Taasisi  ya Wanasheria Wanawake Zanzibar,@ ZAFELA na Center for Youth Dialogue @CYD,wenye lengo la kukuza usawa   wa  kijinsia katika michezo.

 

 

Comments