ZANADAPT.
Waandishi wa habari Kisiwani Pemba wametakiwa kutumia fursa
za mrdi wa ZanAdapt kuwahamasishawanawake kushiriki kwenye demokrasia na uongozi.
Ameyasema hayo Afisa mawasilino TAMWA Zanzibar Nafda Hindi wakati
akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi hao yanayoangazia mabadiliko ya
tabianchi na wanawake.
Akiwakilisha mada ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji kwa
wanawake Ali Mbarouk amesema muda
umefika kwa waandishi kuandaa mikakati itakayohamasisha wanawake kutumia fursa
za mradi kukabiliana na changamoto za tabianchi .
Ameongeza kuna juhudi nyingi zinazochukuliwa na wanawke
katika kukabiliana na tabianchi ikiwemo upandaji wa mikoko na mikarafuu hivyo ni vyema kwa waandishi kutumia kalamu
zao kupaza sauti za wanawake ili kuongeza ushiriki na ushirikishwaji.
Habiba Zarali Rukuni na Is haka Rubea wamesema wanafurahi
kuapata mafunzo ya mabadiliko ya tabianchi na wanawake kwani yatawaongezea
ufanisi katika utekelezaji wa kazi zao.
.Jumla ya waandishi 12 wameshiriki kwenye mafunzo hayo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wa kuandika habari za tabianchi na wanawake yamefanyika Pemba katika ofisi za @TAMWA _Zanzibar.
Comments
Post a Comment